Habari za wakati huu ndugu mpendwa msomaji wa makala za
mtandao huu, ni matumaini yangu kuwa hu mzima wa afya na unaendelea vizuri
kwa kiasi kikubwa sana. Ni matumaini yangu kuwa unaendelea kupambana ilivyo katika kuhakikisha kuwa unatekeleza malengo yako kwa kiwango kikubwa zaidi nami nikusihi kuwa endelea kupambana maana ni muhimu ukayatimiza malengo yako na hapo ndio utaona maana ya kuishi.
kwa kiasi kikubwa sana. Ni matumaini yangu kuwa unaendelea kupambana ilivyo katika kuhakikisha kuwa unatekeleza malengo yako kwa kiwango kikubwa zaidi nami nikusihi kuwa endelea kupambana maana ni muhimu ukayatimiza malengo yako na hapo ndio utaona maana ya kuishi.
Je ulishawahi waza juu ya umuhimu wa kusema hapana?
Nataka nikuambie ndugu msomaji wa makala hii kuwa kuna muda unatakiwa useme
hapana katika maisha yako kama ulikuwa huna tabia hii basi anza kujifunza
kwanzia leo kuwa unahitaji kusema hapana muda mwingine usiwe mtu wa ndio kwa
kila jambo bali tambua kuwa kuna mazingira unahitajika kusema hapana katika
maisha yako. Lazima uishi huku ukiamini kuwa kuna wakati unahitajika kusema
hapana tena kwa nguvu zako zote sema hapana hapana.
Kuna wakati itafika utakuwa unafanya jambo fulani mara
ukapatwa na hali fulani ya kutaka kukata
tamaa, sasa ukijikuta umeanza kufanya jambo fulani alafu ukaijiwa na halli
fulani ya kutaka kukata tamaa hapa ndipo sasa unatakiwa useme hapana, hapana
sito kata tamaa. Na utakaposema hapana utajikuta unaendelea kutenda zaidi na
unapata matokeo uliyokusudia. Kuna stori ya jamaa mmoja ambaye alishindwa
kulitunza shamba lake na hivyo kutokana na sababu zake kadha wa kadha wazo la
kuliuza likamwijia na kwa kuwa alishindwa kujizuia kusema hapana akajikuta
ameuza kumbe shamba lile aliloliuza lilikuwa na madini ya kutosha na aliyenunua
akawa billionea. Hivyo unapohisi unataka kukata tamaa sema hapana na endelea
mpaka upate matokeo uliyokusidia.
Kuna wakati unajikuta unafanya mambo kisa umeambiwa na
watu ambao wanakuzidi umri mfano kaka yako, baba, mama, au dada, bibi au babu.
Sisemi kuwa uwapinge ila nachotaka kukuambia kuwa wakati mwingine unatakiwa
kusema hapana kwao maana mitazamo yao inaweza kuwa hasi yenye kukuangamiza
lakini wewe ukaamua kuifuata na kuishi nayo. Mfano ndugu zako wanakuambia kuwa
si unaona sisi ni masikini hivyo katika ukoo wetu hakuna anayeweza kuwa tajiri
wewe sema hapana mimi naweza kuwa tajiri usikubali kila kitu.
Njoo kwenye mahusiano ni mara ngapi watu wamekuwa
wakifanya mambo ya ajabu tena ya kipuuzi na yasiyo na maana ili tu kuwaridhisha
wapenzi wao. Watu wako tayari kuwadharau hata wazazi wao kuwasaliti ndugu zao
kisa wapenzi wao na hii ni katika kuwaridhisha tu wapenzi wao na kuonyesha kuwa
wanawajali au kama njia ya kulinda mahusiano yao, mfano mpenzi wako wa kiume
anakuambia toroka kwenu leo usiku uje kwangu wakati wewe unajua kuna hatari ya
wewe kushitukiwa hata kabla ujatekeleza hilo jambo, jifunze kusema hapana kwa
mpenzi wako muda mwingine.
Marafiki wanakushawishi kunywa pombe ili hali wewe unajua
pombe ni mbaya na madhara yake mengi unayajua lakini eti kisa kuwaridhisha
rafiki zako unakubali kunywa pombe na hatimaye kuwa mlevi wa kupindukia na
kujikuta unakuwa na maisha mabovu kisa ulevi wako huo, kwanini hausemi hapana
kwa rafiki yako, jifunze kusema hapana
kwa marafiki wenye kukushawishi wewe kufanya mambo usiyoyataka kwa kiwango
kikubwa usihofie kuvunja nao mahusiano.
Kusema hapana sio utovu wa nidhamu na wala sikufundishi
wewe kuwa mtovu wa nidhamu bali nataka uwe na uwazi na ukweli wa kusema hapana
wakati mwingine sio unakubali kubali kupelekwa na watu au hali fulani ya
kimaisha au mwili wako.
Ni mimi rafiki yako,
Baraka Maganga.
Wasiliana nami kwa nambari za simu 0754612413/0654612410 au kwa barua pepe:- Bmaganga22@gmail.com.
No comments:
Post a Comment