Maisha ni mapambano, ni mapambano dhidi ya changamoto
ambazo huibuka kila leo na hatuna budi kuweza kukabiliana na changamoto husika
maana sisi ndio wanajeshi ambao tumejitolea kupambana na adui changamoto ili tuweze kutetea nchi yetu na kushindwa kupambana na adui changamoto kunamaanisha kuwa nchi yetu itavamiwa na tutakuwa mateka wa jumla wa adui yetu mkubwa. Hapa neno nchi yetu limetumika kuwakilisha maisha yetu na mateka wa jumla limetumika kama kuwa masikini. Naamu kushindwa kupambana na changamoto ni kujitakia umasikini.
maana sisi ndio wanajeshi ambao tumejitolea kupambana na adui changamoto ili tuweze kutetea nchi yetu na kushindwa kupambana na adui changamoto kunamaanisha kuwa nchi yetu itavamiwa na tutakuwa mateka wa jumla wa adui yetu mkubwa. Hapa neno nchi yetu limetumika kuwakilisha maisha yetu na mateka wa jumla limetumika kama kuwa masikini. Naamu kushindwa kupambana na changamoto ni kujitakia umasikini.
Tumekuwa tukikumbwa na changamoto mabalimbali na uwezo wa
kupambana na changamoto unabaki kwetu, kila mtu amekuwa na namna yake ya kuweza
kupambana na changamoto ambayo ama kwa nafsi yake huiona kuwa inafaa, lakini
hapa nakuletea njia sita ambazo sio msaada katika kupambana na changamoto hata
kama unazitumiaga na unaona zinafaa lakini changamoto hubaki pale pale. Endelea
kusoma
1. Lawama, hii kwangu ni njia
namba moja ambayo tumekuwa tukiitumia wengi wetu, na wengi wetu huamini kuwa
hii ndio njia sahihi ya kupambana na changamoto zinapotukabili. Lakini leo
nakuambia hii ni njia moja mbaya tena ni namba moja katika ubaya kama kweli
unapambana changamoto. Haifai haifai nakusihi acha acha acha mara moja. Hebu
chukulia wewe ulikuwa mwanafunzi uliye maliza kidato cha nne na baada ya
matokeo kuja unajikuta umefeli vibaya, lakini kuna uwezekano wa wewe kurudia
tena mtihani na ukasonga mbele lakini wewe hulioni hilo badala yake unakaa na
kuanza kuwalaumu waalimu kuwa hawakufundisha vizuri. Nakuuliza hivi kumlaumu
mwalimu kuwa hakukufundisha vizuri kunakusaidia nini? Je kunabadilisha
matokeo?. Umefukuzwa kazi unaanza kumlaumu bosi wakati makosa ni yako, je
kumlaumu bosi kunakurudisha kazini wewe?
2. Visingizio,
namba mbili kwa mujibu wangu katika njia za kukabiliana na changamoto. Utakuta
mtu ni masikini ananza kusingizia ooh mimi niko hivi kwasababu sikusoma, oo
wazazi wangu waliishi kijijini, ooh kwetu hatunaga bahati ya kufanikiwa. Mbona
unapoteza muda wao ovyo kuongelea mambo
ambayo hayana uhusianao na umasikini wako. Na je kusingizia huko sasa
kumekufanya kuwa tajiri sasa?. Acha visingizio wewe ndiye chanzo wa kila kitu
nenda katafute ufumbuzi sio kusingizia.
3. Kulia, nakuona unalia eti
kisa unachangamoto fulani. Nani alikuambia kulia kunatatua changamoto. Kama
unaamini ukilia unatatua changamoto vizuri sana ila nakuambia unajidanganya.
Hebu chukulia mfano unanjaa, njaa imekuuma sana. Njia yako ya kukabiliana na
changamoto si kulia anza kulia sasa kama njaa itaisha. Njaa inatibiwa kwa
kutafuta msosi sio kulia.
4. Kufikiri kujinyonga,
haya ndio mawazo mfu kabisa, umesalitiwa na mpenzi wako eti unataka kujinyoga,
hivi umeiona hiyo ndiyo njia rahisi sana. Hivi ukijinyonga ndio unakuwa
umetatua changamoto au. Aya kama unasema ni sahihi sasa nakuuliza kama kila mtu
angekuwa anakabiliwa na changamoto fulani na anaamua kujinyonga basi dunia hii
ingekuwepo miti tu maana hakuna mtu ambaye hapitiwi na changamoto fulani za
kimaisha. Acha kufikiri kujinyonga sasa.
5. Kuhairisha jambo husika,ukiona
unafanya jambo fulani ukakumbana na ugumu unakimbilia kuacha au kuhairisha
jambo husika, je umeona hiyo ndio njia sahihi sio. Kwahiyo ukihairisha maana
yake utafanya baadae au ukiacha kabisa unakuwa umemamaanisha kuwa utakuwa
umetatua changamoto hiyo?. Huko ni kukimbia majukumu tabia ambayo ni mbovu
sana.
6. Kwenda kuombewa ikiwa huna imani kuwa
itakusaidia, umepigika unajikuta sasa ngoja niende kwa
watumishi nikajaribu kama wanaweza kunisaidia kutatua changamoto hii lakini
sina imani kama wataweza maana, sasa kama huna imani na kitu kwanini ukifanye
sasa, mi naona bora ungeacha kufanya jambo husika. Maana unapoteza muda wako
bure na hautofanikiwa.
Hizo ni njia sita ambazo hautakiwi
kuzifuata ewe mwanamafanikio pindi unapokuwa umekabiliwa na changamoto, lakini
kinyume chake ndio jibu mfano badala ya kulaumu wewe usifanye hivyo badala yake
tafuta njia nyingine.
Ni mimi rafiki yako,
Baraka Maganga.
Wasiliana nami kwa nambari za simu 0754612413/0654612410 au kwa barua pepe:- Bmaganga22@gmail.com.
No comments:
Post a Comment