Katika maisha yetu sisi wanadamu tumekuwa tukiishi na
watu wa aina tofauti tofauti kitabia, kimaumbile na kihali mbalimbali. Yote
haya ni maisha tu
na tunaendelea kuishi katika hali hizi hata kama ikitokea kuwa zinatuletea shida lakini huwa tunajitahidi sana kukabiliana nazo ili tu kutaka kuhakikisha kuwa mambo yanaenda sawa. Haya ndio maisha yetu na huu ndio uhalisia wa maisha yetu yaani hatuwezi kufanana kwa kila kitu maishani.
na tunaendelea kuishi katika hali hizi hata kama ikitokea kuwa zinatuletea shida lakini huwa tunajitahidi sana kukabiliana nazo ili tu kutaka kuhakikisha kuwa mambo yanaenda sawa. Haya ndio maisha yetu na huu ndio uhalisia wa maisha yetu yaani hatuwezi kufanana kwa kila kitu maishani.
Leo sasa nataka kukutahadharisha ndugu msomaji wa makala
hii kuwa usihishi ni kama hakuna maisha tena, hapa nacho maanisha ni kuwa
usihiishi ni kama leo ndio mwisho wako wa kuishi. Binadamu tunaishi tukiwa na
matumaini kuwa kesho tutafika hilo ni jambo jema sana kwetu kwa kuwa na imani
kuwa kesho tutaiona na ndio maana huwa tunajiwekea malengo ya siku, wiki,
mwezi, nusu mwaka na hatimaye tunaweka malengo ya mwaka na hatimaye miaka. Haya ni mambo ambayo wanadamu tumekuwa
tukiyafanya mara kwa mara na kila siku aidha kwa kujua au kuto kujua ila ni
dhahiri kuwa huwa tunayafanya mambo haya.
Leo nataka nikuonye na kukutaadharisha wewe unayeishi ni
kama kesho haitafika yaani unaishi ni kama unakufa leo. Kuna watu wanatabia hii
usinishangae ni kama naongea mambo ambayo hayapo na kama bado hujanipata
endelea kusoma utanielewa tu. Kuna baadhi ya matendo ambayo unaweza kuyatenda
na hatimaye tafsiri yake ikawa ni kuwa unaishi ni kama hakuna maisha tena au ni
kama kesho haifiki matendo hayo ni kama yafuatayo:-
Kuto
kuweka akiba, kuna watu wanaishi pasipo kuweka akiba
maishani mwao yaani yeye kwa kila pesa anayoipata au kitu anachokipata ana tumia
chote bila kujua kesho itakuwaje. Maishani ni muhimu kujiwekea akiba, kama
unatokea kwenye familia za wakulima utakuwa unaelewa fika sana maana ya kuweka
akiba, mkulima baada ya mavuno lazima ataweka akiba ya chakula, nyingine kwa
ajili ya kuuza na mgawanyo utaweza kuendelea. Kwanini mkulima huyu anaweka
akiba ya chakula na hasemi tutumie mazao
yote?, ni kwasababu anajua kuwa kesho ipo ndio maana anaweka. Wewe ni
mfanyakazi ukipata mshahara unatumia wote kiasi kwamba hata ukipata ugonjwa
huwezi kujitibu hii ni hatari sana kwa maisha yako. Jifunze kuweka akiba maana
itakusaidia hapo baadae. Weka akiba usitumie kila kitu ni kama unakufa leo leo.
Wakati nikiwa mtoto mdogo niliwahi kusimliwa na mzee mmoja kuwa kuna mtu baada
ya mavuno ya mahindi yake, alikula chakula akashiba na hatimae akahisi kuwa
kutokana na alivyoshiba hana haja ya kula tena maishani, hatimaye akaamua
kuchoma kihenge chake, lakini kilichomkuta ni kuwa kabla hata kihenge kile
hakijaisha njaa tayari ilikuwa ishamuuma sana. Na hakuweza kupata tena chakula.
Yeye alihisi maisha yanaishia pale ila maisha yaliendelea. Wakati ule nikiwa mtoto
stori hii ilikuwa ya kufurahisha tu lakini leo ina funzo kuwa ni muhimu
kujiwekea akiba maishani usihishi ni kama kesho haipo.
Kuwadhurumu
watu,
kuna watu ni maarufu wa tabia hii lakini wewe unayefanya hivi tambua kuwa sio
kila siku utadhurumu alafu unaweza kuwa ulishawahi kuwadhurumu watu wako wa
karibu na hatimaye ukawa umepoteza uaminifu kwa ndugu zako hao na hatimaye hata
siku ukija kupata shida wakashindwa kukusaidia kitu kutokana na tabia yako ya
kuwadhulumu.
Kusema
uongo, watu wenye tabia hii nao wanaingia hapa katika wale
wanaoishi ni kama kesho haipo, hawa huendelea na tabia yao ya kudanganya lakini
wakishazoeleka watu hupoteza uaminifu kabisa kwao, kuna stori moja juu ya
kijana mmoja ambaye alikuwa mchugaji wa mbuzi katika kijiji kimoja ambacho
kilikuwa jirani na mbuga za wanyama, kijana huyu alizoea kuwadanganya
wanakijiji kwa kupiga kelele za chui kutaka kuwashambulia mbuzi wake hivyo
kelele zake zilikuwa ni zile za kuhitaji msaada lakini mara kwa mara wanakijiji
walipofika walikuta hakuna chui na kijana huyo alikuwa akiwacheka wanakijiji
hao na kujiona mjanja hivyo wanakijiji walizoea kuwa huwa anasema uongo. Siku
ya siku alipiga kelele kumbe siku hiyo chui alikuja kweli na kutokana na uongo
wake kuzoeleka hakuna mwanakijiji aliyekuja kumsaidia na hatimaye mbuzi wake
wakaliwa na chui. Hii ni kwa kuwa alijenga mazoea ya kuwadanganya wanakijiji,
kijana huyu aliishi ni kama hakuna kesho. Alihisi uongo wake utaendelea kila
siku lakini kumbe haikuwa hivyo maana siku hiyo chui alitokea na asijue cha
kufanya.
Usipende kufanya mambo ni kama unakufa leo au ni kama yesu
anarudi leo na kuja kuwachukua watu wake bali ishi huku ukiwaza kuwa kesho ipo
hivyo ujinga, uongo, uzembe na kitu chochote kisicho na maana kinaweza
kukuletea shida kesho na ukashindwa kutatua au ukajikuta upo matatani kutokana
na kuishi ni kama maisha yanaishi leo
leo.
Ni mimi rafiki yako,
Baraka Maganga.
Wasiliana nami kwa nambari za simu 0754612413/0654612410 au kwa barua pepe:- Bmaganga22@gmail.com.
No comments:
Post a Comment