Habari za wakati huu ndugu msomaji wa mtandao huu wa kona
ya maarifa, ni matuimaini yangu kuwa hu mzima wa afya na unaendelea
vizuri katika kupambana na harakati za hapa na pale ili tu kutaka kujiletea mafanikio makubwa zaidi. Vizuri endelea na hali hiyo wala usiache kufanya hivyo, kwa kuwa lengo la mtandao huu ni kukupa elimu juu ya mambo mbalimbali ya kukufanya uweze kufanikiwa basi tuingie katika mada ya leo ambayo ni kuhusu uaminifu.
vizuri katika kupambana na harakati za hapa na pale ili tu kutaka kujiletea mafanikio makubwa zaidi. Vizuri endelea na hali hiyo wala usiache kufanya hivyo, kwa kuwa lengo la mtandao huu ni kukupa elimu juu ya mambo mbalimbali ya kukufanya uweze kufanikiwa basi tuingie katika mada ya leo ambayo ni kuhusu uaminifu.
Uaminifu ni kitu muhimu sana kwa mtu yoyote yule ambaye
anataka kupiga hatua zaidi katika maisha yake husika. Uaminifu ni ile hali ya
kuwa na uwezo wa kutimiza ahadi ambazo
unakuwa umejiwekea mwenyewe. Hii ikiwa na maana kuwa kama ulijiwekea ahadi fulani
au uliweka ahadi fulani na mtu au juu ya mtu au kitu fulani katika maisha yako
na ukaweza kukitekeleza pasipo kuvunja makubaliano sahihi ambayo yaliwekwa au
uliweka hapo tunasema umekuwa mwaminifu. Sasa hapa ntaligawa swala la uaminifu
katika sehemu kuu mbili ambazo ni uaminifu juu yako mwenyewe na uaminifu juu yako na wengine.
Uaminifu juu yako wewe mwenyewe ni ile hali ya kuwa na
uweze wa kutekeleza ahadi ulizojiwekea wewe mwenyewe pasipo kutaka au kuruhusu
ile hali ya kutaka kusitisha sitisha ahadi zile ambazo uliziweka mwenyewe. Tumekuwa
watu wenye kuvunja ahadi ambazo tumekuwa tukijiwekea binafsi katika maisha yetu
na hii inamaanisha kuwa tumekuwa ni watu ambao sio waaminifu sisi kama sisi na
hili limekuwa tatizo kubwa miongoni mwetu. Jiulize ni mara ngapi umekuwa
ukitimiza zile ahadi ambazo umekuwa ukijiwekea wewe binafsi? Jibu la swali hili
litakuwa ni kipimo cha uaminifu wako wewe kama wewe.
Uaminifu baina yako wewe na watu wengine, hapa ndipo
penye shida. Maana uaminifu baina yetu na watu wengine imekuwa ni tatizo sana. Yaani
leo hii ni watu wachache sana kati ya wengi wenye uwezo wa kutunza ahadi kati
yao na watu wengine. Marafiki wengi siku hizi wanagombana na urafiki wao
unavunjika kutokana na ukosefu wa uaminifu baina yao. Ndoa nyingi zinavunjika
kwa sababu ya kukosa uaminifu miongoni mwa wana ndoa husika. Mahusiano mengi leo hii haya dumu kutokana na
uaminifu kukosekana.
Baada ya kusema hayo hapo juu ni muhimu sasa nikakuhasa
ndugu mpendwa msomaji wa makala hii kuwa
jitahidi sana kuwa mwaminifu juu yako wewe mwenyewe na juu ya wenzio. Na
uaminifu wa kwanza ni ule wa kuwa mwaminifu juu yako yaani wewe kama wewe uwe
mwaminifu sasa. Uaminifu utakupanulia uwezo wa kuweza kuaminika na kwa kiasi na
kila mtu. Kuna watu leo hii hawa haminiwi hata na ndugu zao, majirani zao,
marafiki zao kiasi kwamba hata wakipata shida leo hii hawawezi kupewa msaada
wowote kwa kuwa watu hawa hawaaminiki.
Kuna watu leo hii hawakopesheki na taasisi za kifedha
kama vile mabenki na taasisi zingine, achilia mbali taasisi tu hata wale watu
wao wa karibu hawawezi kuwakopesha watu hawa hii ni kwa sababu tu sio waaminifu
watu hawa katika maisha yao. Sasa watu hawa wakati mwingine ndio huanza
kuwatupia watu wengine lawama, kumbe ni wao ndio wamekosa uminifu na matokeo
yake wamejikuta katika shida hizo.
Mimi nikusihi kuwa kwanzia sasa anza kuwa mwaminifu,
jenga uaminifu kwako wewe mwenyewe na baadae kwa watu wengine. Ukiwa mwaminifu
juu yako mwenyewe na wengine pia watakuamini pia.
Ni mimi rafiki yako Baraka Maganga,. Wasiliana nami kwa
nambari za simu 0754612413/0652612410. Au kwa barua pepe ambayo ni
Bmaganga22@gmail.com
No comments:
Post a Comment