Mara nyingi sana tumekuwa watu wenye kukosa hali ya
kuendelea kutaka kufanya mambo ambayo tumekuwa tukitaka kuyafanya. Ukosefu wa
hali hii ndiyo ambayo
hutupelekea sisi kuweza kukata tama ndio maana tumekuwa mabingwa wa kukata tamaa. Sasa ili kuthibiti hali hii nimeona ni bora nikuletee njia tano rahisi ambazo zinaweza kukufanya wewe uwe na hali ya kutaka kuendelea kutenda mambo yako. Zifuatazo ni njia hizo tano:-
hutupelekea sisi kuweza kukata tama ndio maana tumekuwa mabingwa wa kukata tamaa. Sasa ili kuthibiti hali hii nimeona ni bora nikuletee njia tano rahisi ambazo zinaweza kukufanya wewe uwe na hali ya kutaka kuendelea kutenda mambo yako. Zifuatazo ni njia hizo tano:-
1. Fikira chanya,
kuwa na fikira chanya wakati wote, hapa ni kuwa inatakiwa uziondoe fikira hasi
zote katika ubongo wako ili uwe na fikira chanya. Fikira chanya ni muhimu sana
kuliko unavyoweza kudhani maana fikira chanya zitakufanya ufute zile fikira za
kukata tamaa, kushindwa, hofu, woga n.k. fikira chanya ni muhimu sana kama
kweli unataka kufanikiwa maana mtu mwenye fikira chanya huona fursa hata pale
ambapo wengine hawazioni.
2. Jua ni nini unataka maishani, ni
muhimu ujue nini unataka maishani. Usihishi kwa kuwa inabidi uishi badala yake
tafuta kisha utambue ni nini haswa unakitaka maishani. Kujua unachokitaka
maishani kutakupa hamasa kubwa sana kuliko unavyodhani. Nadhani wewe binafsi
unajua hali unayokuwa nayo pindi unapokuwa unajua kitu na pale ambapo unakuwa
haujui kitu. Kujua kitu kunakuwa ni kama kumekupa ramani hivyo basi utakuwa na
hali ya kutaka kutenda mambo.
3. Ifahamu kwanini yako,
hapa nina maanisha kuwa lazima ujue kwanini unafanya jambo fulani, mfano
unapotaka kuwa mwalimu lazima ujiulize kwanini unataka kuwa mwalimu, unapotaka
kuwa daktari lazima ujiulize kwanini unataka kuwa daktari, mwanasheria lazima
ujue kwanini unataka kuwa mwanasheria n.k. Majibu ya maswali haya na mengine
mengi yatakupa hamasa ya kuendelea kufanya kwa kuwa tayari ushajua kwanini
unafanya jambo hilo tofauti na pale ambapo utakuwa unafanya kisa tu unatakiwa
ufanye. Hii ni hatari sana katika nyakati za sasa ambapo mtu anafanya kitu bila
kujua kwanini anafanya hicho kitu. Hivyo basi ifahamu kwanini yako.
4. Tengeneza mpango wa mambo yako, ni
muhimu ukayaendesha maisha yako kwa mipango mathubuti. Usiishi bila mipango hii
ni hatari sana maishani mwako. Pangilia mambo yako hii itakusaidia katika
kufanya mambo yako maana utakuwa unajua wapi uanze wapi umalizie, pia itakupa
uelewa wa ni shughuli ipi uipe kipao mbele sana kuliko nyingine na shughuli ipi
ni muhimu itimizwe mapema kuliko nyingine. Usihishi bila mpango ndugu mpendwa
msomaji wa makala hii. Kuishi bila mpango ni sawa na kuishi kama mfugo ambao
hauna mpango wowote bali unasubiri kufunguliwa bandani au zizini ukale huko kisha
urudishwe na kufungiwa tena bandani ama zizini humo, hii ni hatari kwa binadamu
wa kisasa. Weka weka mipango ya maisha yako.
5. Chukua hatua ndogo ndogo,
waswahili wanasema polepole ndio mwendo hii ni sahihi sana na ndio maana nasema
chukua hatua ndogo ndogo maana ukichukua hatua kubwa kubwa kwa wakati mmoja hii
inaweza kukuletea shida huko mbeleni. Hatua ndogo ndogo hizi zinatoka katika
mipango yako, ndio maana hapo juu nimekusisitiza kuwa weka mipango ya maisha
yako kisha baada ya hapo anza kuchukua hatua ndogo ndogo yaani hapa ni sawa na
kusema anza kufanyia kazi mpango mmoja mmoja na sio yote kwa pamoja hii ndio
maana yangu ya msingi nayo taka kuimaanisha hapa. Chukua hatua ndogo ndogo.
Hizi ni hatua muhimu ambazo ukizifuata
utakuwa umejiepusha katika mtego wa ile hali ya kutaka kukata tamaa. Hivyo basi
fuata njia hizi ambazo ni rahisi na hazi hitaji nguvu nyingi wala muda mwingi
sana. TWENDE SOTE
Ni mimi rafiki yako Baraka Maganga,. Wasiliana nami kwa
nambari za simu 0754612413/0652612410. Au kwa barua pepe ambayo ni
Bmaganga22@gmail.com
No comments:
Post a Comment