Habari za Siku ndugu msomaji wa mtandao huu
wa kona ya maarifa, mtandao ambao umejidhatiti katika kuhakikisha unakupa
maarifa mapya kila Siku na kukusaidia kwa kiasi kikubwa katika kuboresha maisha
yako na kuifanya safari yako ya kuelekea mafanikio isiwe ya kukuchosha na
kukatisha taama. Ambatana nami katika makala ya leo ili ujue leo nimekuletea
kitu gani kipya.
Mara nyingi sana binadamu tumekuwa ni watu wa
kupanga mambo mengi sana juu ya maisha yetu, tumekuwa ni mabwana mipango, na
wengi tumekuwa wenye kuweka mipango mingi sana lakini shida inakuja pale ambapo
inatupasa tutekeleze hiyo mipango yetu. Asilimia kubwa sana ya watu tumekuwa
wenye kuweka mipango mingi na malengo mengi yasiyotekelezeka yaani wengi wetu
mipango yetu na malengo yetu hubaki vichwani mwetu au katika karatasi za
daftari ambamo huwa tunakuwa tumeandika na kuhifadhi mipango na malengo yetu
hayo. Tumekuwa ni kina bwana panga pangua hii ni kutokana na sababu kuwa
tumekuwa tukiweka mipango hii na malengo yale lakini ghafla tunaivunja na
kuweka mipango mingine mipya. Huu umekuwa mchezo wa tulio wengi sana. Je?
Unajua nini kinatufanya tuwe hivyo. Kama haujui basi ambtana nami. Kuna sababu
moja kuu ambayo imekuwa ikifanya hali hii itokee nayo ni kushindwa kujitoa kisawasawa.
Utekelezaji wa mipango na malengo yetu
vinahitaji kujitoa kisawasawa, kupanga malengo yetu na mipango yetu kisha
kuiandika katika vijitabu vyetu vya kumbukumbu zetu haitoshi kutufanya au
kutuonesha wenye mafanikio. Ili utekeleze mipango yako na malengo yako ni
lazima ujitoe kweli. Kuandika malengo au kupanga mipango yako hakukufanyi uwe
mwenye mafanikio bali utekelezaji wa mipango na malengo husika ndio hutuletea
mafanikio.
Baada ya kuwa umepanga malengo na mipango yako
na ukaamua kuitekeleza kisawasawa, ukaanza kuifanyia kazi mipango hiyo lakini
kila unapojaribu kuitekeleza mipango hiyo unajikuta umeshindwa kuitekeleza,
unajaribu tena kwa Mara ya pili unashindwa, unajaribu tena na tena lakini
matokeo yanabaki vile vile. Unajua kwanini hali hii inajitokeza?
Hali hii inajitokeza kwa kuwa ndio umepanga
mipango na malengo yako vizuri lakini hujajitoa kikamilifu katika kuhakikisha
unayatimiza Yale uliyoyapanga, ndio hujajitoa kisawasa pengine unasema hapana
Mimi mbona najituma katika shughuli zangu nafanya hivi na vile ili kutekeleza
yale niliyojiwekea na kujipangia lakini sipati matokeo mazuri kwanini inakuwa
hivi. Jibu ni kuwa hujajitoa kisawasawa.
Unaweza kujiona umejitoa kisawasawa katika
kutekeleza mipango na malengo yako lakini kumbe ndani ya kule kujitoa kwako
kumeambatana na hali ya uvivu hivyo ule uvivu unakufanya usifanye kazi kwa
kiwango kile kinachotakiwa ili kukuwezesha kuyatekeleza Yale malengo yako.
Ikiwa unafanya shughuli zako na unajiona kuwa unaweka jitihada za kutosha
kuyatekeleza Yale uliyojipangia lakini matokeo yanakuja tofauti na ulivyotegema
jua kuwa hujajitoa kisawasawa, kunasehemu ambayo unafanya shughuli kivivu na
ndio maana unashindwa kupata matokeo mazuri.
Endapo utapanga mipango yako vizuri na ukajitoa
kisawasawa basi nakuhakikishia kuwa utafanikiwa kwa kiasi kikubwa hakuna jambo
ambalo litakufanya usipate matokeo Yale ambayo uliyategemea, maana kujitoa
kutakusaidia wewe kuondokana na hali ya uvivu, kukata tamaa na visingizio vya
hapa na pale.
Unapoweka
mipango na malengo yako hakikisha umejitoa kisawasawa katika kuyatekeleza
usiweke tu mipango kisha ukaacha tu mipango inaelea elea, na utambue kuwa
mipango haiwezi kujitekeleza yenyewe.
Ni Mimi rafiki yako.
Baraka Maganga.
Bmaganga22@gmail.com.
0754612413/0652612410.
hongera kwa makala nzuri kaka
ReplyDeleteAsante kaka
ReplyDelete