Tuesday, November 24, 2015

Ni Wewe Wa Kufanya Hakuna Mwingine.


Habari za siku ndugu msomaji wa mtandao huu, ni matumaini yangu kuwa hu mzima wa afya na unaendelea vizuri katika jitihada za kuhakikisha unapambana vikali ili tu kujiletea mafanikio na maendeleo nami nakusihi endelea kuwasha moto huo ulio ukoka ili tu usizime.
Kama kawaida tumekutana hapa lengo ni kutaka kupeana maarifa mapya na leo somo letu/ mada yetu inasema ni wewe wa kufanya na sio mwingine.
Kabla sijaenda mbali nataka ujiulize hili swali je? Unahisi kuna mtu alikuja duniani ili akufanyie jambo Fulani, akupangie mipango, malengo na akuangaikie kila siku ili kutatua matatizo yako. Kama jibu ni hapana, sasa unazani nani yupo ili kufanya kazi zako, kupanga mipango yako, malengo yako n.k. natumaini jibu ni kuwa hakuna mwingine wa kufanya vitu hivyo Bali ni wewe hakuna mwingine bali wewe unaesoma makala hii.
Tambua kuwa kila binadamu anamipango yake, malengo yake, shughuli zake, mawazo yake na fikira zake juu ya maisha yake. Tumekuwa tukiambiana kuwa daaa! Rafiki,ndugu au mwanangu nilikuwa nikikufukiria sana muda mrefu. Hivi unadhani anayekuambia kuwa nilikuwa nakufikiria au anakuwaza aliacha shughuli zako na kuanza kukuwaza tu wewe? Unafikiri wewe unaumuhimu mkubwa sana kwa huyo mtu mpaka aanze kukuwaza wewe sasa kama unategemea au unaamini kuwa kuna mtu anakufikiria umepotea sana tambua hakuna mtu wa kuwazia shughuli zako, wala mikakati yako mingine bali ni wewe mwenyewe yaani usijidanganye kuwa kuna mtu atafikiria juu ya maisha yako hakuna hicho kitu. Atafikiri sawa lakini hawezi kufikiri ama kuwaza kama ambavyo wewe ungefikiri na kuwaza juu ya maisha yako.
Unakaa hutaki kujishughulisha kabisa hutaki kufanya kazi yoyote unategemea watu fulani wakufanyie shughuli hizo hivi unafikiri kuna mtu ni mtumwa wako ambae atakuwa akikufanyia tu shughuli zako huku wewe umekaa tu ukisubiri akufanyie. Unafikiri bado kuna mfumo wa maisha unaoitwa utumwa? Nakuambia hakuna mfumo huo ulikwisha zamani sana pamoja na biashara ya utumwa hivyo leo hii hauwezi kumfanya mtu mtumwa wako kiurahisi. Hivyo tambua kuwa hakuna wa kukufanyia shughuli zako hivyo basi. Inuka ukajishughulishe acha kuona kuwa kuna mtu atakufanyia kazi. Hakuna mwingine wa kukufanyia shughuli bali wewe wenyewe.
Unafikiri kuna mtu maalumu ambaye yupo kwa ajili ya kukupangia malengo yako. Kama unaamini mtu huyo yupo na umempata basi tambua kuwa umepotea na unajidanganya maana hakuna mwingine wa kupanga malengo yako, bali ni we we. Tambua hilo kuanzia leo na ulishike. Malengo bora ni yale ambayo umeyapanga mwenyewe maana utakuwa pindi unapoyasoma yanakuhamasisha na kukumbusha kuwa ni wewe mwenyewe uliye ya panga na kuyaandika hakuna mwingine. Hivyo basi usimruhusu mtu akupangie malengo maana ukifanya hivyo yule anayekupangia malengo ataandika malengo yake na atakuaminisha kuwa hayo malengo ni yako. Hivyo wewe utayafata hayo ukiamini ni yako kumbe umepotea sana tena sana. Hivyo basi tambua kuwa malengo bora ni yale uliyojipangia mwenyewe.
Usipende kujidanganya kuwa fulani ananijali sana huwa anafanya hili na lile kwa ajili yangu, hivyo basi sina haja ya kufanya jambo hilo kwa kuwa kuna mtu yupo anafanya hilo kwa ajili yangu. Nikuulize kitu hivi unauhakika kuwa  huyo anayekufanyia hayo mambo mnaendana kiakili, fikira,mtazamo, ubunifu?n.k. kama jibu ni hapana sasa kwanini unamwachia akufanyie. Acha Mara moja na fanya mwenyewe maana mnatofautiana kiufanisi, ubunifu, akili, uwajibikaji nk.
Ni muhimu utambue kuwa hata ukubwe ma matatizo kiasi gani mwenye nafasi ya kutatua matatizo yako ni wewe na sio mwingine. Una nafasi kubwa sana ya kujihusisha na matatizo na changamoto zinazokukabili tofauti na mtu mwingine yoyote. Hivyo basi wa kuwajibika na changamoto zako ni wewe sio mwingine. Daktari pekee hatoshi kukuponya ila uwepo wa daktari na imani yako ndio vitu vya kukuponya wewe hata kwa yale magonjwa yanayoonekana hayawezekani kutibika.
Tambua kuwa haukuja duniani ili ufanyiwe kitu Fulani. Bali ulikuja duniani ili ufanye jambo au mambo Fulani. Hivyo basi kuanzia leo tambua kuwa hakuna mwingine wa kukufanyia bali ni wewe mwenyewe.
Ni Mimi rafiki yako,
Baraka Maganga.
Bmaganga22@gmail.com.
0754612413/0652612410.


No comments:

Post a Comment