Wednesday, November 25, 2015

Ifahamu Aina Ya Mbegu Unayoipanda.


Habari ndugu msomaji wa mtandao huu wa kona ya maarifa ni matumaini yangu kuwa hu mzima wa afya. Na unaendelea kupambana vikali katika shughuli zako ili tu kuhakikisha kwamba unajiletea mafanikio makubwa. Nami nakuambia vizuri pia nakusihi endelea kupambana mpaka pale utakapo timiza malengo yako. Kama kawaida kila tunapokutana hapa huwa tunakutana kwa lengo moja tu nalo ni kupeana maarifa mapya. Leo jambo nalo taka kukushirikisha ni kuhusiana na upandaji wa mbegu.
Naposema upandaji wa mbegu najua kuna wale ambao mawazo yao yatawatuma kuwa nataka kutoa darasa juu ya upandaji wa mbegu za aina fulani shambani, na kuna wale ambao watabaki na mshanga kuwa namaanisha nini haswa. Usiwe na haraka ndugu msomaji bali endelea kuisoma makala hii kisha utanielewa ni mbegu gani namaanisha. Binadamu tumekuwa wapanda mbegu wakubwa sana tena sana maana hakuna siku ambayo inapita bila sisi kupanda mbegu hizi. Lakini tofauti ya mbegu hii na ile ya zile mbegu tulizozoea kupanda mashambani sio kubwa sana ila utofauti upo tu katika mahali pa kupandia. Yaani zile mbegu za shambani tunazipanda shambani au kuzifukia ardhini. Lakini hii mbegu nayo kuletea ni mbegu inayopandwa katika ubongo wa mwanadamu yaani kichwani au akilini mwa binadamu. Nisikuache nyuma ndugu msomaji wa makala hii utakapo kuwa unasoma makala hii na kukuta neno mbegu jua neno hili linasimama au nimelitumia badala ya neno fikira. Hivyo naposema unapanda mbegu gani namaanisha kuwa unajijengea fikira gani? Nadhani mpaka hapo utakuwa umeanza kunipata sasa. Sasa mbegu tunazopamba zimegawanyika katika makundi makuu mawili ambayo ni kama ifuatavyo:-
Mbegu mbovu, /fikira mbovu (hasi), neno mbovu si neno geni kwako ndugu msomaji lakini japokuwa unaielewa maana yake lakini mimi nataka kuielezea au kulielezea neno mbovu zaidi kwako. Tunaposema kuwa kitu Fulani ni kibovu, kwa tafsiri ya haraka haraka ni kuwa tunamaanisha kuwa kitu hicho hakifai kwa matumizi. Na kama hakifai kwa matumizi maana yake ni kuwa haupaswi kukitumia kabisa kwa namna yoyote. Na pindi ukikitumia basi chaweza kukuletea madhara makubwa sana hebu chukulia mfano wa madhara ambayo unaweza kuyapata kutokana na kula chakula kibovu au kilichoharibika, wakati mwingine waweza hata kupoteza maisha. Turudi katika uhalisia sasa, hapa kwa wale ndugu zangu wakulima nadhani mtanielewa zaidi, hivi toka lini mtu akaipanda mbegu mbovu na akategemea mavuno mengi ya kuzii?. Unajua ni kwanini wakulima huchambua mbegu zao kabla ya kuzipanda au unajua ni kwanini wakulima huitaji mbegu bora? Jibu ni rahisi wakulima uchambua mbegu nzuri ili wasipande mbegu ,bovu kwa kuwa wanajua kuwa mbegu mbovu kamwe haiwezi kuzaa matunda na kama ikizaa matunda hayo yatakuwa mabaya.

Sasa chukua mfano huu wa mbegu mbovu ubadilishe jina lake na mifano yake, yaani badala ya mbegu mbovu weka fikira mbovu (hasi). Kwanini ulalamike usiku kucha, mchana kutwa kuwa maisha magumu, maisha hayaendi kila unachofanya hakieleweki na unakalia kumlaumu mungu kuwa kawapendelea wengine nk. Kumbe tatizo ni fikira zako mbovu ndizo zinakuletea matatizo yote hayo. Kama ilivyo katika mbegu kuwa mbegu mbovu haizai basi hata katika fikira ni hivyo hivyo nini cha kufanya sasa cha kufanya ni kufutilia mbali fikira mbovu.
Mbegu bora /fikira njema(chanya), mbegu bora ni ile yenye kuzaa matunda mengi tena kwa wingi sana, hii ni mbegu ambayo haina  takataka za aina yoyote yaani ni mbegu ambayo ni safi sana na hivyo mpandaji huipanda pasipo kuwa na wasiwasi wowote ule juu ya uotaji na kipato. Hivi ndivyo ilivyo hata kwa fikira njema au chanya, mtu mwenye fikira chanya hana wasiwasi na maisha yake maana anaamini kuwa karanga iliyopandwa huzaa karanga inayofanana na mbegu husika na wala karanga haiwezi kuzaa mchungwa. Fikira njema haina takataka kama vile woga, ukataji tama, uhairishaji wa mipango ovyo vyo, majungu wala upotezaji wa muda ovyo.
Ni vyema ukajijengea fikira njema au chanya ili usiishi kwa wasiwasi, chagua mbegu bora ili uwe na uhuru na masiha yako. Ikiwa unaishi tu pasipo kuchagua aina ya mbegu inayokufaa basi aina yoyote ile ya matokeo kubaliana nayo lakini nakutaadharisha na uzingatie kuwa hauwezi kuvuna ambacho hukupanda hivyo chunguza matokeo ya mambo yako kisha utajua aina gani ya mbegu umepanda. Nakutakia kila kheri katika safari yako ya kuyaelekea mafanikio.
Ni mimi Rafiki yako,
Baraka maganga.
Bmaganga22@gmail.com
0754612413/0652612410.


No comments:

Post a Comment